WASANII wa Kundi la Kaole, Mariamu Athuman ‘Kalunde’ na Herry Mohamed
‘Niko’ wamepata ajali na kuumia vibaya baada ya gari walilokuwa
wakisafiria kupasuka tairi na kuacha njia.
Ajali hiyo ilitokea
hivi karibuni maeneo ya Kiteto mkoani Manyara ambapo wasanii hao ambao
ni wapenzi, walikuwa wakitumia gari aina ya Vogue wakielekea kwenye
msiba. Walikuwa watu watano kwenye gari hilo ambao wote walijeruhiwa
sehemu mbalimbali.
No comments:
Post a Comment