Powered By Blogger

Tuesday, May 21, 2013

INASIKITISHA SANA, HIVI NDIVYO KIJANA ALIVYOMUUA BABA YAKE SIKU YA HARUSI YA MDOGO WAKE, SOMA HAPA

SAKATA la kijana Bonny Fabian Kavishe kudaiwa kumuua kwa kumpiga risasi baba yake, mzee Livingstone Kavishe akiamini ni mwizi sasa ni simulizi ya machozi kufuatia kusomwa kwa waraka mzito ulioandikwa na mtuhumiwa huyo ambaye bado yupo mahabusu ya Polisi Mlandizi, Bagamoyo, Pwani.,,,,,Waraka huo ulizidi kuwatoa machozi baadhi ya waombolezaji siku ya mazishi yaliyofanyika Marangu, Wilaya ya Moshi Vijijini, Mkoa wa Kilimanjaro kutokana na maneno yenye huruma ya Bonny kuomba msamaha.
WARAKA ULIANDIKIWA NDANI YA MAHABUSU
Habari zisizo na chenga wala kumulika tochi zinasema, mtuhumiwa akiwa mahabusu aliamua kuandika waraka huo na kumpa ndugu yake mmoja (jina halikupatikana) akimpa maelekezo kwamba usomwe siku ya mazishi ya mzee huyo kabla hajafukiwa kaburini kwa vile yeye hatakuwepo.
“Kwa kweli inauma sana! Jamaa alipoona hatapata ruhusa ya askari ili akashiriki mazishi ya baba yake aliomba karatasi na kalamu na kuandika waraka, akampa ndugu yake mmoja, akamwambia usomwe siku ya mazishi ya marehemu kabla hajafukiwa kaburini,” kilisema chanzo......MWILI WAAGWA NYUMBANI KWA MTUHUMIWA, WASAFIRISHWA NA WARAKA
Jumatano ya Mei 15, mwaka huu, mwili wa marehemu mzee Kavishe uliagwa nyumbani kwa mtuhumiwa licha ya yeye kutokuwepo na ukasafirishwa kwenda Marangu kwa mazishi.
Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa kwenye kusafirisha mwili huo ni uwepo wa waraka huo ambao mtuhumiwa aliomba usomwe mbele ya waombolezaji siku ya mazishi.
MANENO NDANI WARAKA NI HAYA
Siku ya mazishi, mwanaume aliyepewa jukumu la kuongea kwa niaba ya familia aliusoma waraka huo huku waombolezaji wakiwa makini kumsikiliza.
Alisema waraka huo umeandikwa kwa mikono ya Bonny Kavishe, licha ya kuzungumzia mambo mengine, aliwaomba msamaha ndugu, jamaa na marafiki kwamba wamsamehe kwa kitendo cha kumuua baba yake.
Alisema alifanya kitendo hicho bila kukusudia na wala hajui nini kiliendelea. Haikuwa nia yake kumtoa uhai baba yake aliyefikia nyumbani kwake Mlandizi kwa ajili ya kusherehekea harusi ya mdogo wa mtuhumiwa huyo iliyofanyika Mei 11, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment