Powered By Blogger

Saturday, May 18, 2013

PROFESA JAY; NA SAKATA LA JIDE VS RUGE

Funguka: Mambo vipi Profesa, nimekutafuta ili nipate msimamo wako kwenye bifu kati ya msanii mwenzako (Jide) na Ruge.
Profesa Jay: Kwanza nianze kusema kuwa mimi sina upande wowote ambao ninaweza kuusimamia, sipo kwa Ruge wala kwa Jide.
Funguka: Kumekuwa na minong’ono mitaani kuwa upo upande wa Jide kwani mmekuwa mkifanya kazi pamoja vilevile ni marafiki kwa muda mrefu na ndiyo maana amekushirikisha kwenye wimbo wake wa Joto Hasira. Unalizungumziaje hili?
Profesa Jay: Ishu siyo mimi kuwa upande wa Jide au wa Ruge, kitu ambacho ninaweza kukizungumzia ni kwamba Jide alinishirikisha kwenye wimbo huo hata kabla ya hilo bifu lao sijalifahamu. Mimi niliimba kutokana na maudhui ya wimbo ulivyokuwa ukitaka. Kwa hiyo bado nasisitiza kuwa sifungamani na upande wowote katika jambo hili.
Funguka: Kama ni hivyo, unachukuliaje suala la Jide na Ruge kufikia hatua ya kuburuzana mahakamani?
Profesa Jay: Kuhusu hilo, sitakuwa msemaji sana ila kwa jinsi ninavyofahamu, Jide ni msanii mkongwe. Kama unakumbuka nilishawahi kufanya naye traki kadhaa kama Bongo Dar-es-salaam na Niamini. Kikubwa ni kwamba Jide anajiheshimu sana na nadhani kila anachokifanya anakijua vizuri.
Funguka: Unamuongeleaje Ruge na uongozi mzima wa Clouds kuhusu sakata hili?
Profesa Jay: Binafsi siwezi kuwaongelea Clouds au Ruge kwa jambo lolote, kwa sababu ninaamini na wao ni watu wazima na wanafahamu nini wanachokifanya.
Funguka: Hivi karibuni tumesikia wasanii kadhaa wamejitoa kwenye orodha ya wasanii watakaomsapoti Jide kwenye shoo yake ya Mei 31, vipi wewe utakamua kama kawaida?
Profesa Jay: Nikutoe wasiwasi, mimi binafsi nitakuwepo kwenye shoo ya Jide na nitapiga mzigo wa kufa mtu kumsapoti kwa akili yangu yote, nguvu zangu zote na moyo wangu wote.
Funguka: Poa, nashukuru kwa ushirikiano wako, kazi njema.
Profesa Jay: Haina kwere.

No comments:

Post a Comment