Powered By Blogger

Wednesday, May 15, 2013

MATONYA AUVAA MSALA WA JIDE

WAKATI wasanii wa Bongo Fleva, Elias Barnaba na Estalina Sanga ‘Linah’ wakidaiwa kupokea fedha na kuitolea mbavuni shoo ya Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee’ au Jide, msanii Seif Shaban ‘Matonya’ naye ameuvaa msala mpya wa kuikacha shoo hiyo huku akiminyia mshiko wa kianzio (advance) aliolipwa tangu  mwishoni mwa Aprili, mwaka huu.

Kwa mujibu wa mtandao wa Lady Jaydee, Matonya alikuwa miongoni mwa wasanii watakaopafomu katika shoo ya kuadhimisha miaka 13 ya Lady Jaydee inayotarajia kufanyika Mei 31, mwaka huu katika Ukumbi wa Nyumbani Lounge, jijini Dar lakini baadaye akagaili.

No comments:

Post a Comment