WAKATI wasanii wa Bongo Fleva, Elias Barnaba na Estalina Sanga ‘Linah’
wakidaiwa kupokea fedha na kuitolea mbavuni shoo ya Judith Wambura Mbibo
‘Lady Jaydee’ au Jide, msanii Seif Shaban ‘Matonya’ naye ameuvaa msala
mpya wa kuikacha shoo hiyo huku akiminyia mshiko wa kianzio (advance)
aliolipwa tangu mwishoni mwa Aprili, mwaka huu.
Kwa mujibu wa
mtandao wa Lady Jaydee, Matonya alikuwa miongoni mwa wasanii
watakaopafomu katika shoo ya kuadhimisha miaka 13 ya Lady Jaydee
inayotarajia kufanyika Mei 31, mwaka huu katika Ukumbi wa Nyumbani
Lounge, jijini Dar lakini baadaye akagaili.
No comments:
Post a Comment