Powered By Blogger

Saturday, June 1, 2013

RAIS OBAMA KUFUNGA HOTELI YA NYOTA 5 KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM


Wakati Rais wa Marekani, Barrack Obama akitarajiwa

 kuwasili na msafara wa watu 700, baadhi ya hoteli zenye 
hadhi ya nyota tano jijini Dar es Salaam zimeanza 
kusitisha kupokea wageni kutokana na ujio huo.

Taarifa iliyotolewa na Ubalozi wa Marekani ilisema 
Rais huyo, anatarajiwa kuwasili nchini Julai Mosi kwa 
ajili ya ziara ya siku tatu hadi Julai 3 mwaka huu ili 
kuimarisha uhusiano baina ya nchi hiyo pamoja na nchi 
za Afrika. Msafara huo utajumuisha watu mbalimbali 
wakiwamo wafanyabiashara.

No comments:

Post a Comment